Soma Biblia ni nani?

Soma Biblia Society ni shirika la wahisani linalolenga kusambaza Injili ya Yesu Kristo kwa rika zote. Shabaha nyingine ni kuwasaidia Wakristo kufikisha Injili kwa watu na kuwafundisha kupitia neno la Mungu – juu ya imani na maisha. Tazama baadhi ya kazi zetu hapa chini

Kusambaza Biblia, Vitabu na Vifaa

Tuna maduka na magari yanayosambaza Biblia za watu wazima na za watoto, vitabu vya Kikristo na vifaa vya Madhabahuni.

Agiza Biblia

Tunachapisha Vitabu vya Kikristo

Tunaandaa na kuchapisha vitabu vinavyokusaidia kukua katika mafundisho ya Neno la Mungu, kukua katika imani na maisha ya Kikristo.

Nunua Vitabu

Soma Biblia kwa Njia ya Mtandao

Huduma ya kusoma vitabu vyetu kwa manufaa zaidi. Kozi hii ni bure isipokuwa gharama ya kitabu tu. Yupo mwalimu wa kukushauri.

Jiunge na Kozi

Uinjilisti na Misheni

Tunaendesha programu za vijana (Fikia Maisha Chaguo ni lako), Tunafanya uinjilisti maeneo mbalimbali na kuwafikia wale ambao bado hawajamjua Yesu Kristo.

Jiunge nasi

Soma Biblia App

Huduma ya kununua, kusoma, kusikiliza, kutazama na kujifunza Neno la Mungu popote ulipo kidijitali. Ni rahisi kutumia, ina Kiswahili na Kiingereza na maktaba ya bure.

Pakua App

HABARI KUTOKA SOMA BIBLIA

SOMA BIBLIA APP

Neno la Injili
Kiganjani Mwako

Pakua Soma Biblia App leo na uweze kununua Biblia, Vitabu vya Kikristo, Vifaa vya Madhabahuni, kutazama video na kusikiliza shuhuda katika simu yako.

📖

Nunua Biblia

Nunua Biblia na vitabu vya Kikristo kwa urahisi.

🎧

Sikiliza

Sikiliza mafundisho na shuhuda za kukutia moyo.

🎥

Tazama

Tazama video za Soma Biblia kuhusu mafundisho ya Neno la Mungu.

🎓

Jifunze

Jiunge na kozi za Biblia kwa njia ya mtandao.

Pakua Soma Biblia App
Soma Biblia App

Mawasiliano

Idara ya Mauzo

Kama ukitafuta kitabu na bei yake, au kutaka kuagiza na kununua vitabu

Simu: +255 754 292 995 
Baruapepe: manager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 12772, Dar es Salaam, Tanzania              

Makao: Barabara ya Mwai Kibaki, Mikocheni B, upande wa pili wa Sanitas Medical Centre. Maduka yanapatikana Dar es Salaam (Mikocheni B & Mbezi Luis), Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma na Iringa

Idara ya Uchapishaji

 Ukiwa na mswada au kutaka Soma Biblia kusambaza kitabu chako.

Simu: +255 787 392 951
Barua Pepe: publishingmanager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 2696, Arusha, Tanzania                  

Makao: Eneo la Sakina, upande wa pili wa sheli ya mafuta ya Oryx (kituo cha basi huitwa Oil Com). Fuata kibao cha Scripture Mission.

“Niliona moja ya kipeperushi chenu kikiwa chini maeneo ya stendi ya mabasi. Kimebadilisha maisha yangu.”

— Mtu Mmoja Alisema