Soma Biblia ni nani?
Soma Biblia Society ni shirika la wahisani linalolenga kusambaza Injili ya Yesu Kristo kwa rika zote. Shabaha nyingine ni kuwasaidia Wakristo kufikisha Injili kwa watu na kuwafundisha kupitia neno la Mungu – juu ya imani na maisha. Tazama baadhi ya kazi zetu hapa chini
Kusambaza Biblia, Vitabu na Vifaa
Tuna maduka na magari yanayosambaza Biblia za watu wazima na za watoto, vitabu vya Kikristo na vifaa vya Madhabahuni.
Agiza BibliaTunachapisha Vitabu vya Kikristo
Tunaandaa na kuchapisha vitabu vinavyokusaidia kukua katika mafundisho ya Neno la Mungu, kukua katika imani na maisha ya Kikristo.
Nunua VitabuSoma Biblia kwa Njia ya Mtandao
Huduma ya kusoma vitabu vyetu kwa manufaa zaidi. Kozi hii ni bure isipokuwa gharama ya kitabu tu. Yupo mwalimu wa kukushauri.
Jiunge na KoziUinjilisti na Misheni
Tunaendesha programu za vijana (Fikia Maisha Chaguo ni lako), Tunafanya uinjilisti maeneo mbalimbali na kuwafikia wale ambao bado hawajamjua Yesu Kristo.
Jiunge nasiSoma Biblia App
Huduma ya kununua, kusoma, kusikiliza, kutazama na kujifunza Neno la Mungu popote ulipo kidijitali. Ni rahisi kutumia, ina Kiswahili na Kiingereza na maktaba ya bure.
Pakua AppHABARI KUTOKA SOMA BIBLIA
Neno la Injili
Kiganjani Mwako
Pakua Soma Biblia App leo na uweze kununua Biblia, Vitabu vya Kikristo, Vifaa vya Madhabahuni, kutazama video na kusikiliza shuhuda katika simu yako.
Nunua Biblia
Nunua Biblia na vitabu vya Kikristo kwa urahisi.
Sikiliza
Sikiliza mafundisho na shuhuda za kukutia moyo.
Tazama
Tazama video za Soma Biblia kuhusu mafundisho ya Neno la Mungu.
Jifunze
Jiunge na kozi za Biblia kwa njia ya mtandao.
Mawasiliano
Idara ya Mauzo
Kama ukitafuta kitabu na bei yake, au kutaka kuagiza na kununua vitabu
Simu: +255 754 292 995
Baruapepe: manager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 12772, Dar es Salaam, Tanzania
Makao: Barabara ya Mwai Kibaki, Mikocheni B, upande wa pili wa Sanitas Medical Centre. Maduka yanapatikana Dar es Salaam (Mikocheni B & Mbezi Luis), Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma na Iringa
Idara ya Uchapishaji
Ukiwa na mswada au kutaka Soma Biblia kusambaza kitabu chako.
Simu: +255 787 392 951
Barua Pepe: publishingmanager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 2696, Arusha, Tanzania
Makao: Eneo la Sakina, upande wa pili wa sheli ya mafuta ya Oryx (kituo cha basi huitwa Oil Com). Fuata kibao cha Scripture Mission.
“Niliona moja ya kipeperushi chenu kikiwa chini maeneo ya stendi ya mabasi. Kimebadilisha maisha yangu.”
— Mtu Mmoja Alisema
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kusema hapana kwa yale yasiyo mapenzi ya Mungu. Makala zote zitatutia moyo na kutujengea ujasiri wa kusema hapana. Mfano mzuri ni Danieli na rafiki zake walivyomwambia Mfalme (tazama uk.15). Kwa vijana kuna makala muhimu sana juu ya kutunza miili yetu. Na usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. TSH. 500 TU.